Muhammad Baqir Qalibaf amesema kuwa fikra za Imam Khomeini (M.A) na Mapinduzi ya Kiislamu katika miongo iliyopita zilikuwa na manufaa makubwa ambapo hivi sasa tumesimama imara mkabala wa adui mwenye nguvu. Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran amebainisha hayo leo katika hafla ya kufunga duru ya pili ya uteuzi wa athari zilizofanya vizuri katika harakati ya muqawama na kulinda haram tukufu ambayo hufanyika kila baada ya miaka miwili.
Qalibaf ameongeza kuwa suna ya Mwenyezi Mungu na wananchi wenye imani ni kigezo kile cha kujitetea kutakatifu cha walinzi wa haram ambacho kimepatikana katika eneo na kuweza kupigana vita na Daesh katika hali ambayo hakuna jeshi lolote lililoweza kukabiliana na kundi hilo la kigaidi.
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa walinzi wa haram ni vikosi na askari ambao wanachama wake wametoka katika vijiji na miji mbalimbali katika Ulimwengu wa Kiislamu na kisha kujumuika pamoja chini ya maktaba ya Uislamu na Qurani Tukufu.